Malengo
Maendeleo ya Taifa letu yataletwa na wananchi wenye afya bora
inayowawezesha kuzalisha mali na kutoa huduma mbalimbali. Katika miaka
mitano ijayo.
Serikali itachukua hatua za kuboresha, kuimarisha na hata kupanua elimu ya
Awali hadi ya Chuo Kikuu na kuhakikisha kwamba elimu ya ngazi zote
itakayotolewa nchini tangu sasa iwe ya ubora utakaowawezesha vijana wetu
kuchukua nafasi zao stahiki katika Jumuiya ya Afrika Mashariki...
Katika kipindi cha miaka mitano ijayo ya utekelezaji wa Ilani ya 2010-2015,
Chama kitazielekeza Serikali kutekeleza kwa ukamilifu malengo ya Mpango wa
Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP) pamoja na kaulimbiu ya Kilimo
Kwanza inayotoa msukumo katika kutekeleza mambo mbalimbali.
Katika kipindi cha utekelezaji wa Ilani hii, Chama kitaielekeza Serikali iendelee
kuitangaza hazina ya utalii tuliyonayo kwa mbinu za kisasa ili kukuza zaidi
mchango wa utalii kwa pato la Taifa kwa kutekeleza yafuatayo:-
Katika kipindi cha Ilani hii ya miaka 2010-2015, Chama Cha Mapinduzi
kitazielekeza Serikali kuiendeleza sekta ya mifugo kwa ari zaidi, nguvu zaidi na
21
kasi zaidi ili kuiwezesha kutoa mchango mkubwa kwenye pato la Taifa kwa
kuchukua hatua mbalimbali.
Katika kipindi cha utekelezaji wa Ilani ya miaka ya 2010 – 2015, Chama
kitaielekeza Serikali kuyalinda na kuyaendeleza mafanikio kwa kuchukua hatua
zifuatazo:-
Katika miaka mitano ya utekelezaji wa Ilani ya 2010 – 2015, Chama kitaitaka
Serikali kuongeza kwa kiwango kikubwa uzalishaji wa nishati ya umeme kutoka
MW 1051 hadi MW 1722 (sawa na ongezeko la MW 671) na kupunguza ile ya
tungamotaka kwa kuchukua hatua zifuatazo:-
Mwelekeo wa Sera za CCM katika miaka ya 2010 hadi 2020 umeainisha jukumu kubwa la nchi yetu katika kipindi hiki ni kutekeleza lengo la Dira 2025...
Katika kipindi cha utekelezaji wa Ilani hii ya 2010 – 2015, Chama Cha Mapinduzi
kitaitaka Serikali iikuze sekta ya viwanda kutoka asilimia 9.9 ya sasa hadi asilimia
15 mwaka 2015 kwa kuweka mazingira mazuri kwa ajili ya maendeleo endelevu
ya sekta za viwanda, biashara na masoko kwa kuzingatia mambo yafuatayo:-
Kutokana na umuhimu wa Sekta ya Umwagiliaji katika kukuza uchumi wa taifa
na wa wananchi katika kipindi hiki kwa kuongeza uhakika wa upatikanaji wa
chakula nchini, Chama kitaitaka Serikali kutekeleza yafuatayo:-










